• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

AWESO ATOA SIKU 14 DAWASA KUPELEKA MAJI MTAA WA GOLANI, KIMARA

Posted on: December 24th, 2020

Waziri wa Maji  Jumaa Aweso  ametoa  siku 14 kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja kufikisha huduma ya maji kwa wananchi wa mtaa wa golani kata ya kimara baada ya kukosa huduma hiyo kwa muda mrefu. 


 Agizo hilo ametoa leo tarehe 24 desemba,2020 alipotembelea na kukagua mradi mpya wa maji unaotekelezwa katika  mtaa wa Golani kata Kimara jimbo la Ubungo   na kueleza kuwa huduma ya maji ni ya msingi na haina mbadala hivyo  naiagiza DAWASA kukamilisha mradi huu ndani ya siku 14 ili wananchi wa golani wapate maji.

Waziri wa Maji Jumaa Aweso akizindua uchimbaji wa mtaro kwa ajili ya kutandika mabomba ya maji kwenye mradi mpya wa maji Golani  kata ya kimara leo alipotembelea kata hiyo. 


Katika Ziara hiyo, waziri wa maji aliongizana na Waziri wa Uwekezaji  Prof. Kitila Mkumbo ambaye ni mbunge wa jimbo la Ubungo , mbunge wa kibamba Issa Mtemvu na viongozi mbalimbali wa wilaya  ya ubungo. 


Aweso ameeleza kuwa "Pamoja na kazi kubwa mnayoifanya DAWASA ya kusambaza maji katika jiji la Dar Es Salaam lakini maeneo ya pembezoni kama golani mnayasahau , nawakumbusha kuwa kila mtanzania ana haki ya kupata huduma ya maji  safi na salama na ndio ahadi ya serikali "


Aidha waziri Aweso amewataka watendaji wa DAWASA  kufainyia kazi malalamiko ya wateja wao kwa haraka kwani kwa kufanya hivyo wananchi watafurahia huduma zenu badala ya kuzipuuzia au kuzichukulia kimazoea "Wananchi wanahitaji huduma ya maji na bila maji wananchi wanatumia muda na gharama kubwa kupata maji chapeni kazi"


Aidha mhe. Waziri amewataka wananchi wa  golani kuwajibika kulipa bili za maji , kulinda na kutunza miundombinu ya maji pindi mradi huo utakapokamilika ili mradi uwe endelevu.

Wananchi wa Golani wakimsikiliza kwa makini Waziri wa maji  Jumaa Aweso (hayupo pichani) wakati alipotembelea mtaa huo kutatua kero ya maji iliyodumu kwa muda mrefu.


Nae Mbunge wa Jimbo la ubungo Prf. Kitila Mkumbo ambaye pia ni Waziri wa Uwekezaji amewahakikishia wananchi wa Jimbo hilo kuwa serikali itaendelea kutatua kero za wananchi ikiwemo changamoto ya barabara za pembezoni ili ziweze kupitika vizuri tofauti na hali ya sasa.

Mbunge wa Jimbo la ubungo  mhe Prof Kitila Mkumbo ambaye pia ni waziri wa Uwekezaji akishiriki uchimbaji wa mtaro kwa ajili ya kuweka mabomba ya maji ili kupeleka huduma ya maji Golani.

Kwa upande wake Afisa mtendaji mkuu wa DAWASA  mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa kazi ya kulanza bomba la maji lenye urefu wa kilomita 3.7 kwa mradi wa golani imeanza na ndani ya Siku 14 wananchi watapata maji kama alivyoelekeza Mhe. Waziri.


Mhandisi Luhemeja amefafanua kuwa, Kutokana na jografia ya golani kuwa na milima na mabonde mengi, huduma ya kuunganisha maji majumbani haitakuwepo badala yake yatapatikana kwenye viosi pekee.
Aidha mhandisi luhemeja amesema  changamoto ya maji kwa maeneo ya pembezoni imeanza kufanyiwa kazi ampapo DAWASA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali  yenye zaidi ya bilioni 100. Patikanaji wa maji kwa Wilaya ya ubungo upo kwa asilimia 45 

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa