• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

BARAZA LA MADIWANI UBUNGO LAPITISHA MAKISIO YA BAJETI YA TSH BILIONI 109.4

Posted on: February 10th, 2023


Baraza la Madiwani Manispaa ya Ubungo limepitisha makisio ya mpango wa bajeti ya Halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2023/2024 yenye jumla ya Tsh 109,449,392,100 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ruzuku ya mishahara na matumizi mengineyo.

Baraza limepitisha mapitio hayo kwenye mkutano maalumu wa baraza la Madiwani uliofanyika leo februari 10, 2023 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo na kuweka msisitizo wa kusimamia ukusanyaji wa mapato ili kufikia malengo.

Akiwasilisha rasimu ya makisio ya mpango na bajeti ya Halmashauri hiyo Ndg. Andambike Kyomo Mchumi wa Manispaa hiyo alifafanua kuwa jumla ya bajeti hiyo ya shilingi 109,449,392,100 imejumuisha shilingi 74,838,346,000 ambayo ni ruzuku kutoka Serikali kuu, shilingi 34,520,402,100 ni fedha za makusanyo ya ndani ya Halmashauri na shilingi 90,644,000 ni fedha kutoka kwa wafadhili.

Kyomo ameendelea kufafanua kuwa kiasi cha shilingi 74,838,346,000 ambacho ni fedha za ruzuku kutoka Serikali kuu zinajumuisha kiasi cha shilingi 62,341,057 ikiwa ni mishahara, shilingi 1,278,545,000 kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi 11,218,744,000 kwa ajili ya miradi ya maendeleo toka Serikali kuu.

Kiasi cha Shilingi 34,520,402,100 ambacho ni fedha ya mapato ya ndani inajumuisha kiasi cha shilingi 22,059,738,000 ni mapato halisi, kiasi cha shilingi 11,635,664,100 ni mapato lindwa na kiasi cha shilingi 825,000,000 ni michango ya wananchi.

Sambamba na hayo Kyomo amesema bajeti hiyo imazingatia vipaumbele sita ikiwemo kuboresha makusanyo ya mapato ya ndani, kuboresha miundombinu ya elimu, uboreshaji wa huduma na miundombinu sekta ya afya, kuimarisha utawala bora, kuboresha miundombinu ya barabara na kuimarisha usimamizi, ufuatiliaji na utoaji taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Akihitimisha Mhe. Nyaigesha amemshukuru Mhe Rais kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo na uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya 10% na kuahidi kuwa bajeti ya 2023/2024 Manispaa itaenda kutekeleza miradi itakayoenda kutatua kero za wananchi katika nyanja mbalimbali

Aidha, Mstahiki Meya amesema ukusanyaji wa mapato utafanyika kwa ufanisi kwa kila mtu kushiriki ipasavyo na kusimamia sheria ndogo mpya za Manispaa hiyo  

“Kwa mara ya kwanza Halmashauri yetu inaanza kutumia sheria ndogo zake mpya ambazo zimetungwa na baraza la Manispaa ya Ubungo badala ya zile za Kinondoni ambazo tulikuwa tukizitumia muda wote” alisema Mstahiki Meya.

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa