• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

BODI YA AFYA MANISPAA YA UBUNGO YAFANYA KIKAO CHA ROBO YA PILI 2019/2020

Posted on: February 11th, 2020

Bodi ya Afya ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo leo imefanya kikao cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

Kikao hicho kimefanyika hospitali ya Sinza kikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi  Ndg. Israel Sosthenes  na Katibu wa Bodi ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Manispaa  Dr. Peter Nsanya. pamoja na wajumbe wa bodi. Akiongea kwenye kikao hicho Mwenyekiti aliwaambia wajumbe kuwa kuna umuhimu wa bodi kutembelea miradi ya Afya ili kujionea hali halisi.

Mwenyekiti pia alisisitiza suala la ulinzi katika mradi wa Hospitali ya Wilaya. Alisema kuwa kuna haja ya kuhakikisha kuna ulinzi wa kutosha ili kudhibiti aina yoyote ya wizi au utoroshaji wa vifaa vya ujenzi unaoweza kujitokeza.

’’Niitake sasa idara ya Afya kuhakikisha maagizo yanayotolewa na bodi au Idara kwenda kwenye Zahanati na Vituo vya Afya yanakuwa kwenye maandishi” aliongeza Mwenyekiti.

Vile vile Mwenyekiti aliwaomba wajumbe kusisitiza wananchi kujiunga na Bima ya Afya ili waweze kupata matibabu na dawa kwa uhakika zaidi. Sambamba na hilo alimtaka Mganga Mkuu kuandaa mkakati wa kuelimisha wananchi juu ya faida za kujiunga na Bima ya Afya.

Ndg. Sosthenes pia alitilia mkazo suala la kuongeza mapato kwenye vituo vya Afya na zahanati, kusimamia na kutumia vizuri mapato yake katika kuboresha huduma kwa wananchi.

Nae Mganga Mkuu aliihakikishia bodi kuwa eneo ambalo hospitali ya Wilaya inajengwa ni salama na lina ulinzi wa kutosha.

Mganga Mkuu aliitarifu bodi kuwa kuanzia tarehe 14 hadi 28 mwezi huu Idara ya Afya itashirikiana na kanisa katoliki kutoa huduma za kibingwa katika kituo cha Afya Kimara, Zahanati ya Goba na Kituo cha Afya Mbezi. Baadhi ya vipimo vitakavyotolewa ni upimaji wa tezi dune na saratani ya shingo ya kizazi *’’HUDUMA HII ITAKUWA BURE NA ITAHUSISHA MADAKTARI BINGWA’’*

Mwenyekiti ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya *Mhe. Dr. John Pombe Magufuli* kwa ushirikiano wanaoutoa kwa miradi ya Afya na kuahidi kumpa Mhe. Rais ushirikiano.

Akifunga kikao Mwenyekiti aliwashukuru wajumbe kwa ushirikiano lakini alisisitiza kuwasimamia vizuri watumishi wa idara ya Afya vile vile kuhakikisha watumishi wanakuwa waadilifu na kujitolea kwa dhati ili wananchi wetu waweze kupata huduma bora.


Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa