• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DC MAKORI AIAGIZA MANISPAA YA UBUNGO KUKAMILISHA MRADI WA JENGO LA UTAWALA

Posted on: December 30th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo mhe Kisare Makori ameiagiza Manispaa ya Ubungo kuongeza kasi ya umaliziaji wa jengo la utawala la Manispaa hiyo ili  kurahisha utoaji huduma kwa wananchi pamoja na kuwa na mazingira mazuri ya kufanyia kazi kwa  watumishi wa Manispaa hiyo.

Mhe. Makori ametoa agizo hilo leo tarehe 30 desemba,  2020 wakati alipotembelea na kukagua utekelezaji wa mradi huo  akiwa ameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo na  kueleza kwamba Serikali ya awamu ya tano inahitaji miradi itekelezwe kwa wakati  na  kwa kuzingatia viwango lengo ikiwa nikurahisisha utoaji huduma kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo mhe. Kisare Makori (mwenye t-shirt ya mistari) akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi  na usalama wa wilaya hiyo pamoja na wataalamu wa Manispaa ya Ubungo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kukagua utekelezaji wa jengo la Ofisi za Utawala Manispaa ya Ubungo leo tarehe 30.12.2020

"Baada ya kuvunja mkataba na TBA kutokana na ucheleweshaji wa mradi, Manispaa imewapa  kazi nyinyi local fundi ili mradi uishe kwa wakati lakini utekelezaji wenu bado unasuasua, naagiza kufikia tarehe 7 januari  2021 kila fundi awe amemaliza kazi aliyopewa kwa mujibu wa mkataba wake "alieleza Mhe Makori

Kwa upande wake Mkurugenzi  wa Manispaa ya Ubungo, Beatrice  Dominic alisema kuwa Manispaa itajitahidi kuwasimamia mafundi  kufanya kazi usiku na mchana ili kufikia  januari  2021 kazi zote ambazo zinafanywa kwa sasa ziwe zimekamilika na jengo kutumiwa katika hali ya utulivu.

Beatrice ameeleza kuwa kwa sasa kazi zinazofanyika ni uwekaji wa Umeme, mifumo ya maji taka, ufungaji wa milango na upakaji rangi. Kazi zote mafundi wapo wanafanya kazi na fedha zipo " tutajitahidi kuwasimamia wafanye kazi kwa muda tuliokubaliana"

Ili kuhakikisha kazi zote zinafanyika kwa usahihi na ubora unaotakiwa, Beatrice  alieleza kuwa Manispaa  ya Ubungo imetafuta wataalamu mshauri  kwenye masuala ya umeme na uwekaji wa mifumo ya TEHAMA ambaye atashirikiana na mafundi kuhakikisha kazi hizo zinafanyika kwa viwango vinavyotakiwa.

Mradi huo unajengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 6.2 ambapo kati  ya fedha hizo  bilioni 1.9 kutoka mapato ya ndani na zaidi  ya bilioni 4 ni fedha kutoka serikali Kuu. 

Jengo la Utawala  la Manispaaya Ubungo likiwa kwenye hatua za umaliziaji. 

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa