• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DC UBUNGO ARUDISHA ENEO LA SHULE LILILOVAMIWA NA MWANANCHI

Posted on: July 17th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kisare Matiko Makori amemaliza sintofahamu ya nani ni mmiliki halali wa eneo la zaidi ya ekari moja la Shule ya Sekondari Goba Mpakani iliyopo Kata ya Goba Mtaa wa Tegeta A.

Katika ziara yake hiyo Mkuu wa Wilaya aliambatana na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo  Ndg. James Mkumbo , Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo  Beatrice Dominic  na wataalam kutoka Manispaa hiyo.

Kabla ya Mkuu wa Wilaya kutatua mgogoro huo alimtaka Kaimu Afisa Mipango miji wa Manispaa Ndg. Fadhili Hussein kutoa historia fupi ya eneo hilo.

Aidha Kaimu Afisa Mipango Miji wa Manispaa alisema kwamba eneo lote tayari wananchi wameshalipwa fidia na eneo ambalo limevamiwa lilikuwa linamilikiwa na Ndg. Ally Chande ambaye tayari alishalipwa Tsh. Milioni 314. Baada ya hapo mtu anayefahamika kama Kisoki alimuuzia eneo hilo hilo kitapeli mtu anayefahamika kwa jina la Kapama.

Aliongeza kuwa kuna makosa yalifanyika katika kupatiwa hati kwani Kapama ana hati ambayo aliipata kimakosa kwa kujua au kutokujua.

Baada ya maelezo hayo  Mhe. Kisare  alisema mambo matatu, Moja eneo sio la Kapama bali ni la Shule, Pili amepewa hati kwenye eneo ambalo tayari limeshafidiwa na Serikali. Tatu Kapama hatokaa aendeleze eneo hilo kwa sababu ni la Serikali.

Pia aliongeza kuwa kuna utaratibu wa kisheria ambao ulitumika kwenye utoaji wa hati na utaratibu huo huo utatumika kuona namna ya kufuta hati hiyo.

Sambamba na hayo aliwaomba wananchi kutoa taarifa kama eneo hilo litaendelezwa kwa namna yoyote kwani wao ndio wapo karibu na eneo hilo na tayari mhusika ameitwa mara kadhaa bila ya kuitikia wito huo na ana notisi ya kutoendeleza eneo.

Katika ziara hiyo wananchi walieleza kero wanazozipata kwenye maji, elimu, ulinzi na Usalama na mpaka wa Tegeta A na Kulangwa.

”Namuagiza Afisa Mipango Miji hadi kufikia Jumatano ya tarehe 22 mwezi huu mgogoro wa mpaka wa Mtaa wa Tegeta A na Kulangwa uwe umeisha kwani michoro ipo na pamoja na hilo ashughulikie mgogoro wa mpaka wa Matosa na Tegeta A.” aliongeza DC.

Katika suala la Ulinzi na Usalama DC alisema amesikia kilio cha wananchi kwa adha wanayoipata ya kufuata huduma mbali kutokana na kukosa kituo karibu na aliwachangia kiasi cha *Tsh. Milioni 1* kuendeleza ujenzi wa kituo.

Elimu, Mkuu wa Wilaya wa Wilaya alimuagiza pia Afisa Mipango Miji kuangalia kama eneo la Sekondari linatosha kujenga Shule ya Msingi ili Shule hiyo ijengwe kuwapungizia watoto kwenda mbali kwa ajili ya kupata elimu na kukutana na changamoto nyingi barabarani.

Wakati akifunga mkutano huo na wananchi Mkuu wa Wilaya alisisitiza suala la amani hasa wakati huu wa uchaguzi, vile vile wananchi wachague viongozi ambao watakuwa bega kwa bega kumsaidia Mhe. Rais Magufuli kuleta maendeleo na wanaokereketwa na kero zao na sio wanaowakimbia baada ya kuchaguliwa kama walivyofanya wengine wa upinzani.

”Niwaombe wajasiriamali wadogo mkachukue vitambulisho vya wajasiriamali ili mfanye biashara popote pale bila kubugudhiwa” Alisisitiza Mkuu wa Wilaya.


Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa