• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

DC UBUNGO AWATAKA DAWASA KUFUATA RATIBA ZA MGAO WA MAJI UBUNGO

Posted on: November 10th, 2022


- Leo Novemba 10, 2022 Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kheri James amefanya kikao kazi kati ya wenyeviti wa serikali za mitaa na Mameneja wa DAWASA Wilaya ya Ubungo ili kufanya tathmini ya changamoto ya maji iliyopo sasa pamoja na kuweka mikakati ya kumaliza changamoto hiyo kwa Wilaya ya Ubungo

- Katika kikao hicho James amesema kuhusu tatizo la maji linaloikumba Dar es Salaam kwa sasa ni lazima kwanza kukubali kuwa tatizo lipo kisha kuendelea kutekeleza mikakati ya kumaliza tatizo hilo ambalo limesababishwa na kupungua kwa kina cha maji katika mto Ruvu.

- Kwasasa serikali imekuja na mpango wa kuchimba na kufufua visima vya maji ambavyo vitaongeza maji kwenye mfumo mzima wa DAWASA na kupelekea ahueni kwa wananchi

- Wakiongea katika kikao hicho baadhi ya wenyeviti wa Serikali za mitaa wamesema kuwa DAWASA ihakikishe inatekeleza ratiba ya mgao walioweka na kama kutakua na mabadiliko ya ratiba hiyo kuwe na taarifa mapema ili wananchi waelewe

- Aidha kwa upande mwingine James amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mikakati aliyoelekeza kukabiliana na tatizo hili la maji ikiwemo mpango wa kufufua visima kale na kuchimba visima vipya ambapo siku ya kesho Rais Samia anatarajiwa kukabidhi mitambo kwaajili ya kuchimba visima hivyo katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Ubungo na Dar es Salaam kwa ujumla
"Mhe. Rais anafanya kazi kubwa sana kukabiliana na tatizo la maji kwa Dar es salaam nzima. Wenyeviti muwe wa kwanza kutambua na kumtia moyo Mhe. Rais kwa kazi nzuri na kubwa anayoifanya" Alisema

- Wakati kikao hicho kikiendelea, Mhe. Mkuu wa wilaya alifanya mawasiliano kwa njia ya simu na Waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso ambapo amewaondoa hofu wenyeviti hao kuhusu tatizo la maji ambalo juhudi zinaendelea kufanyika kupunguza adha hiyo. Aweso pia amewapongeza mameneja wa DAWASA kwa wilaya ya Ubungo kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya kukabiliana na changamoto hii.

- Akijibu hoja za Wenyeviti Meneja wa DAWASA Kibamba ndugu Elizabeth Sankere amesema kuwa hoja zote wamezichukua na wameahidi kuzifanyia kazi haraka sana kutoka sasa. Kwa upande mwingine Sankere amewapongeza wenyeviti hao kwa kutoa ushirikiano kwa DAWASA

@dawasatz

#ubungoyetufahariyetu
#dawasa

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa