• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

HALMASHAURI YA MANISPAA YA UBUNGO YAWATAKA WAMILIKI WA VIBANDA SOKO LA SHEKILANGO NA SINZA KULIPA KODI KULINGANA NA BEI ELEKEZI

Posted on: May 11th, 2020

Afisa Biashara wa Manispaa ya Ubungo Prisca Mjema  wakati akitoa ufafanuzi kuhusiana na bei iliyowekwa na Manispaa kama malipo ya kodi ya vibanda vya soko la Shekilango na Sinza.

Akiongea na waandishi wa habari Afisa Biashara alisema kuwa  Manispaa imekuwa ikipoteza mapato mengi katika vibanda vya masoko hayo kwa kukusanya mapato kidogo kulinganisha na hali halisi ya maeneo yaliyopo.

Aliongeza kuwa bei iliyopangwa ya Tshs.150,000 imewekwa kwa mujibu wa sheria ndogo ndogo za Halmashauri na vile vile imezingatia bei halisi ya upangishaji katika maeneo husika.

"Niwaombe wafanyabiashara wawe waelewa na kama kuna jambo hawajalielewa basi ofisi zetu zipo wazi kwa ajili ya kutoa ufafanuzi na  Kama watalipa kodi kwa majibu wa mkataba basi Manispaa itaongeza mapato na kuweza kujenga miundombinu mizuri katika masoko yetu, kujenga masoko mapya, kujenga madarasa na maendeleo mengine". Alifafanua Afisa Biashara.

Nae Meneja Masoko wa Manispaa *Ndg. Geofrey Mbwama* alisema kwa soko la Shekilango lina jumla ya vibanda 293 na wanaolipa kodi ni vibanda 27 tu, soko la Sinza lina vibanda 192 na wanaolipa kodi ni vibanda 97 tu hali ambayo inapelekea Manispaa kupoteza mapato mengi.

Aliongeza kuwa katika vibanda hivyo wajenzi wengi wamevipangisha kwa wafanyabiashara wengine kinyume na sheria lakin pia wamekuwa wakiwatoza kodi kuanzia Tshs 80,000 hadi Tshs.600,000 kwa mwezi wakati Manispaa ikipokea 15,000 tu.

Aidha kwa  utafiti na mazungumzo yaliyofanyika kati ya Manispaa na waliojenga vibanda mambo kadhaa yalibainika, Wajenzi wengi walikuwa hawana nyaraka wala gharama halisi, Wajenzi wote hawana mikataba kutoka Manispaa ya Ubungo, Hakuna ramani za wajenzi wa vibanda, waliojenga sio wanaofanya biashara bali wengi wao wamewapangisha watu wengine kinyume cha sheria na taratibu.

Mwisho Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Beatrice Dominic aliwaasa wamiliki wa vibanda hivyo kuweza kukubaliana na kulipa kiasi kilichopangwa kwa mujibu wa sheria kwa maendeleo ya wanaubungo na watanzania kwa ujumla katika kuleta maendeleo.

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa