• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

KAMATI YA FEDHA UBUNGO YAFANYA ZIARA YA KIKAZI DODOMA JIJI

Posted on: June 3rd, 2022

Kamati ya Fedha na  Uongozi Manispaa ya  ubungo pamoja na wataalamu wakiongozwa na Mstahiki Meya Mhe. Jaffary Juma Nyaigesha imefanya ziara ya mafunzo katika Halmashauri ya jiji la dodoma, lengo ikiwa ni kupata uzoefu wa ujenzi wa mabanda ya wamachinga kutokana na jiji hilo kufanya vizuri katika kutekeleza mradi huo.


Ziara hiyo ni utekelezaji wa agizo la Waziri Ofisi ya Rais  TAMISEMI  Mhe. Innocent Bashungwa alipotembelea Kituo cha Mabasi cha Magufuli mwishoni mwa mwezi Mei ambapo moja ya kero iliyojitokeza ni  mazingira ya wamachinga kutoendana na mahitaji yao.

Akizungumza  baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa mabanda ya kisasa ya machinga jijini humo, mstahiki Meya wa Manispaa ya ubungo ameeleza kuwa ziara hiyo imewapa mwanga mzuri wa namna ya kwenda kutekeleza mradi wa ujenzi wa mabanda ya wamachinga kwa ubora na usasa zaidi.


Pamoja na mradi wa ujenzi wa mabanda ya machinga, jiji la dodoma pia linatekeleza miradi mikubwa ya  kimkakati ikiwemo masoko, Hoteli, ukumbi na maeneo ya kupumuzikia ambayo ni miradi ya uwekezaji na inayoliingizia jiji mapato ya ndani kwa uhakika.


Baadhi ya miradi iliyokamilika ikiwemo soko, stendi na maeneo ya wazi  tayari jiji linakusanya fedha kutoka kwenye Miradi huku miradi ya ujenzi wa hoteli mbili za kisasa ukiwa hatua nzuri za ukamilishaji.

Mradi wa ujenzi wa Soko la machinga

Akiieleza kamati ya fedha ya Ubungo siri ya mafanikio hayo Mstahiki meya wa Jiji la Dodoma Dkt Mwamfupe alisema kuwa udhubutu wa maamuzi, ushirikiano na ushirikishaji wadau ndio vimepelekea mafanikio  hayo ya kuweza kuwa na miradi mikubwa ya uwekezaji ikiwa ni suluhisho la kuwa na vya uhakika wa mapato na kupelekea kutoa huduma bora kwa wananchi.


Dkt  Mwamfupe anasema "Haya mafanikio sio fedha ni udhubutu wa kuamua kufanya jambo linaloweza kuwezesha jiji kutoa huduma kwa kutumia fedha za mapato ya ndani bila kutegemea fedha za Serikali Kuu lakini  pia ni vyanzo vya uhakika"

Mradi wa ujenzi wa Ukumbi wa kisasa eneo la Mtumba

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa