• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

KAMATI YA SIASA WILAYA YA UBUNGO YAFURAHIA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA MANISPAA YA UBUNGO

Posted on: June 19th, 2020

 Kamati ya siasa Wilaya ya Ubungo imefanya ziara yake kukagua miradi ya maendeleo katika Wilaya hiyo tarehe 19/06/2020.

Katika ziara hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Chama Wilaya ya Ubungo Ndg.Lucas Mgonja, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe.Kisare Makori, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Beatrice Dominic na kuhudhuriwa na Katibu tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg.James Mkumbo na viongozi mbalimbali wa chama cha Mapinduzi, Vyama rafiki vya upinzani na Wataalam kutoka Manispaa ya Ubungo.

Katika ziara hiyo Miradi iliyotembelewa ni Mradi wa ujenzi wa barabara ya Shekilango, Mradi wa ujenzi wa kingo za mto Ng'ombe kilomita 8.5 na Mto kiboko kilomita 3.5, Mradi wa ujenzi wa daraja la juu Ubungo (Flyover), Mradi wa ujenzi wa mabanda 7 ya wajasiriamali Mbezi luis uliopo Kata ya Mbezi na Mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Amani iliyopo Kwembe na dhumuni kuu likiwa ni kuona maendeleo ya miradi hiyo.

Aidha viongozi wa Chama Wilaya walipongeza juhudi ambazo zimefanywa na Wataalam waliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo kwa usimamizi mzuri wa miradi.

"Napenda kumshukuru raisi wetu wa awamu ya tano Dr.John Pombe Magufuli kwa maendeleo ambayo amefanya katika Wilaya yetu ya Ubungo na Tanzania kwa ujumla kwa kuboresha maendeleo ya wananchi wote"  Alisema Mkuu wa Wilaya.

Sambamba na hilo  Mkuu wa Wilaya alivishukuru vyama rafiki vya upinzani kwa heshima waliyoitoa na kuungana na uongozi wa Wilaya na Kamati ya siasa CCM ya Wilaya.

Pia Mkuu wa Wilaya aliwahakikishia wajumbe kuwa miradi ambayo walishindwa kufika imeakisi miradi ambayo imetembelewa.

Nae Mwenyekiti wa ACT wazalendo Wilaya kwa niaba ya vyama vingine aliushukuru uongozi wa Wilaya ya Ubungo ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya kwa ushirikishwaji wao.

"Niseme wazi Wilaya ya Ubungo ni Wilaya ya kuigwa kwani ndio ya kwanza kushiriki kwenye ziara ya kutembelea miradi na vyama vingine." Alisisitiza Mwenyekiti wa ACT

Aliongeza kwamba vyama vya upinzani vipo tayari kushirikiana na vyama vingine kwa maslahi ya Taifa.

Wakati akifunga Mwenyekiti wa CCM Wilaya alimpongeza Mkuu wa Wilaya na Wakuu wa Idara kwa kazi nzuri wanayoifanya kutekeleza miradi.

"Niwaombe wakati wa kupiga kura kumchagua Rais wote tukampigie kura John Pombe Magufuli kwa maendeleo ya Taifa letu na kwa kuzingatia Rais wetu kila siku anasisitiza maendeleo hayana chama."


Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa