• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MANISPAA YA UBUNGO YAFANYA KIKAO NA WADAU WA ASASI WALIOPO KATIKA MANISPAA HIYO

Posted on: July 10th, 2020

Kikao hicho kilifanyika   katika ukumbi wa Tunu Hall uliopo Mbezi na kuongozwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi ambaye pia ni Kaimu mkuu wa idara ya Maendeleo ya jamii  Mercy Ndekeno  Mratibu wa asasi zisizo za Kiserikali  Manispaa ya Ubungo  Juliana Kibonde na kuhudhuriwa na wawakilishi wa Asasi mbalimbali zilizopo Manispaa ya Ubungo  na Wataalam kutoka katika Manispaa hiyo.

Lengo la kikao hicho ni utambuzi wa asasi ambazo zipo Manispaa ya Ubungo na kutathimini shughuli zinazofanywa na asasi  hizo na kutengeneza mpango kazi utakao tumika kwa mwaka 2020/2021

"Ni lazima asasi zifanye kazi zake kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu ambazo zitasaidia katika kuhakikisha mnafanya kazi za kuhudumia wananchi ipasavyo na lengo kutimia, pia mhakikishe mnapata kibali kutoka Tamisemi kitakachosaidia asasi zenu kutambulika." Alisema hayo Juliana Kibonde

"Kazi zikafanyike kwa weledi na mkahakikishe mnasimamia misingi yenu ya kazi ili kufanikisha maendeleo ya asasi zenu na kuleta maendeleo katika Manispaa ya Ubungo"Aliongeza Juliana

Aidha mwakilishi wa dawati la Ukimwi Manispaa ya Ubungo ambaye pia ni kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii  Mercy Ndekeno aliwaasa kuhakikisha wanatoa elimu kuhusu magonjwa yanayoikumba jamii kwa sasa na kama watekelezaji wa asasi hizo kuwa mstari wa mbele kuhamasisha jamii kujitokeza kupima magonjwa mbalimbali kama ukimwi, shingo ya kizazi n.k

Pia Mwakilishi wa dawati la vijana Bi.Bupe Mwansasu aliwaomba wahakikishe katika asasi zao wanaendesha mafunzo kuhusu stadi za maisha kwa jamii na kushirikiana na wadau kuanzisha vituo vya ushauri nasaha na kuendeleza vipaji vya vijana walioko katika jamii.

Sambamba na hayo Juliana alizungumzia kuhusu dawati la Mtoto na wanawake  ambalo Idara ya Maendeleo ya jamii inashughulika nalo kuhakikisha mtoto anapewa haki zake na mwanamke katika jamii kutambua haki zake na kuepeukana na manyanyaso na ukatili wa kijinsia.

Nae mwakilishi wa asasi ya Family Walfare Foundation  Angela Mfinanga ameshukuru kwa elimu waliyoipata  na maandalizi yaliyofanyika ya kikao hicho.

Mwisho  Mercy Ndekeno  aliwashukuru kwa ujio wao na  kuwakaribisha tena  Manispaa ya Ubungo.







Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa