• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MANISPAA YA UBUNGO YAJIPANGA KUONGEZA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: December 17th, 2020

Manispaa ya Ubungo jijini Dar Es Salaam imeweka mikakati madhubuti ya  kuongeza ukusanyaji wa  mapato ya manispaa hiyo kwa kuongeza juhudi za usimamizi wa vyanzo vilivyopo pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato lengo ikiwa kupandisha mapato kutoka bilioni 18  mpaka kufikia angalau bilioni 20 kwa mwaka.


Mikakati hiyo imejadiliwa  leo kwenye kikao cha kujadili namna bora ya kuongeza makusanyo ya mapato ya manispaa hiyo kilichojumuisha waheshimiwa madiwani , wakuu wa idara na vitengo pamoja na watendaji wa kata na mitaa  ambapo kila kata imewasilisha mikakati ya namna ya kuongeza mapato kwa kuimarisha vyanzo vya mapato.

Wajumbe wakifuatilia majadiliano ya namba ya kuongeza mapato ya manispaa ya Ubungo


Akizungumza wakati akifungua kikao hicho,  Mustahiki Meya wa Manispaa hiyo  Jaffary Nyaigesha amesema kuwa Manispaa ya Ubungo ina uwezo wa kukusanya mapato makubwa zaidi kuliko inavyokusanya sasa ikiwa tu viongozi na watendaji wa manispaa  tutashirikiana kwa pamoja kusimamia ukusanyaji wa mapato.



Mtahiki Meya ameeleza kuwa, Vyanzo vya mapato vinavyotakiwa kusimamiwa ni pamoja na vibali vya Ujenzi, Kodi za ardhi, ushuru wa huduma, kuimarishwa ukusanyaji wa mapato kwenye masoko pamoja na kutengeneza mazingira mazuri ya kufanyia biashara kwa ajili ya kuvutia uwekezaji,ukuaji wa biashara ndogondogo na za kati na hatimaye kuongeza mapato.

Mheshimiwa Diwani wa Kata ya manzese akitoa mchango wa namna ya kuboresha ukusanyaji wa Mapato ya manispaa ya Ubungo.


“Manispaa ya Ubungo inapoteza mapato mengi sana kutokana na mianya mingi ya uvujishaji mapato kutokana na usimamizi mdogo au baadhi ya viongozi


 Kwa upande wake Diwani wa kata ya Sinza   ameeleza kuwa , Pamoja na kubuni vyanzo vya mapato na kusimamia ukusanyaji wa mapato, wajumbe wa kikao wameadhimia kuongeza utoaji wa elimu ya mlipa kodi ili wafanyabiashara watambue umuhimu wa kulipa kodi kwa hiyari “ tumieni vyombo vya habari ikiwemo radio za kijamii pamoja mitandao ya kijamii ambayo imeonekana kutumiwa zaidi kupata taarifa mbalimbali”


Aidha, Mkurugenzi wa Manispaa Beatrice   Dominic  ameeleza kuwa Manispaa inaendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kielektroniki ambapo jumla ya PoS 130 zinatumika kukusanya mapato katika vyanzo mbalimbali ikiwa njia ya kuhakikisha mapato ya Manispaa hayapetei, pia Manispaa iko kwenye mchakato wa kununua PoS 100 Kwa lengo la kuimarisha ukusanyaji wa mapato.


Pia, Beatrice amesisitiza watendaji wa kata na Mitaa kusimamia kwa dhati ukusanyaji wa mapato pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato ili Manispaa isipoteze mapamapato


Watendaji wa kata na mitaa wakisikiliza kwa makini Kikakati ya kuongeza ukusanyaji wa mapato

"Tunapaswa kuwajibika Kwa pamoja ili kuongeza Kasi ya ukusanyaji wa Kodi na tozo mbalimbali ili tuboreshe utoaji wa huduma kwa wananchi ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo" alisisitiza Beatrice


Kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Manispaa ya Ubungo ilikasimia kukusanya bilioni 18 na mapaka sasa imefanikiwa kukusanya  Zaidi ya 45%.


Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa