• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MANISPAA YA UBUNGO YAKABIDHI VITI NA MEZA 200 KWA AJILI YA KIDATO CHA KWANZA

Posted on: January 8th, 2021

Ikiwa  zimebaki Siku chache kufunguliwa kwa shule, Manispaa ya Ubungo leo januari 8, 2021 imekabidho madawati 200 shule za sekondari  ambazo zina upungufu wa viti na meza ikiwa ni maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa  kidato cha kwanza kwa mwaka 2021.

Akizungumza wakati wa kukabidhi viti na meza hizo, Afisa elimu wa Manispaa hiyo Hilda sharanda amesema kuwa Manispaa imekabidhi viti na meza hivyo 200 kwa shule za sekondari ikiwa ni moja ya mkakati wake wa hukakikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza kutoshindwa kusoma kwa sababu ya ukosefu wa viti na meza.

Sharanda ameeleza kuwa,   Wanafunzi wote 13, 347 walichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza watasoma katika mazingira mazuri kwani Manispaa imetoa fedha shilingi milioni 115  kwa ajili ya kutengeneza viti na meza ambapo kwa leo tu akabidhi viti na meza hizi 200 huku vingine 1000 ikiwa hatua za mwisho za matengenezo

Kwa ujumla, shule zina upungufu wa viti na meza 2847 kati ya 10500 vilivyopo ambapo katika upungufu huo viti 1200 vinatengenezwa na Manispaa kupitia mapato ya ndani,  1000 vimefanyiwa ukarabati shuleni hivyo tunaendelea kuomba wadau wengine waendelee kutusaidia ukizingatia elimu ni sekta mhimu sana kwa ustawi wa jamii na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wa vyumba cha madarasa , sharanda amesema kuwa   wanafunzi 13,347 waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza wanahitaji vyumba cha madarasa  268 lakini vyumba 231 vipo na hivyo  kufanya upungufu wa vyumba 37

Aidha, sharanda amesema,   katika kukabiliana na upungufu huo manispaa imetoa fedha milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba cha madarasa 37 ambapo utekelezaji wake upo hatua mbalimbali lengo ikiwa ni kuhakikisha wanafunzi wote walichaguliwa kuanza kidato cha kwanza  hawaikosi furss hiyo kutokana na ukosefu wa madarasa ya kusomea.

Kutokana na juhudi hizi za Manispaa na  serikali kwa ujumla, sharanda amewataka wazazi na walezi wahakikishe wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wanaripoti shule kwa wakati wakiwa na mahitaji yote ya msingi kwani mazingira ya kujifunzia yako vizuri yaani Walimu, madarasa na madawati.

Akiongea wakati wa kukabidhiwa viti na meza kwa ajili ya kidato cha kwanza Mwalimu Andrea Ndagire kutoka shule ya sekondari Kibweheri ameishukuru serikali kupitia Manispaa ya Ubungo kwa kutoa viti na meza hizo kwani vitapunguza kwa Miesi kikubwa upungufu uliokuwepo shuleni mwaka

Aidha Mwalimu Ndagire ameeleza kuwa kitendo cha Manispaa ya hiyo kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kutatua changamoto katika sekta ya elimu ni kutekeleza kwa vitendo Dhana ya uchumi wa kati kwa vitendo maana wanafunzi anakuwa katika mazingira mazuri ya kujifunzia na hivyo kuwa na Taifa bora ukizingatia elimu ni msingi wa ustawi wa sekta zingine.

Walter priscus prosper ni moja ya wanafunzi walichaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika shule ya sekondari kimara, ameipongeza serikali  kwa kutoa viti na meza kwenye shule zake ili wanafunzi wasome katika mazingira mazuri.

"Kwa niaba ya wanafunzi wenzangu tunaahidi kusoma kwa bidii ili fedha zinazotumika kujenga miundombinu ya shule pamoja na utoaji wa elimu bila malipo zisipotee bure" aliahidi mwanafunzi prosper.

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa