• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MANISPAA YA UBUNGO YAKABIDHIWA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA SHIRIKA LA OCODE

Posted on: October 23rd, 2022



Shirika la OCODE TANZANIA limekabidhi chumba kimoja cha darasa la mfano kwa ajili ya wanafunzi wa awali, viti 16, meza Tatu na zana za kufundishia vyenye thamani ya shilingi milioni 39 katika Shule ya msingi Kiluvya iliyopo Kata ya Kibamba Manispaa ya Ubungo lengo ikiwa ni kuhamasisha wanafunzi kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Akiongea katika hafla hiyo ya kukabidhi miundombinu hiyo Mkurugenzi wa OCODE  Bw. Joseph Jackson amesema sambamba na ujenzi huo wamefanikiwa kutoa mafunzo ya mbinu na zana mbadala za kufundishia iitwayo jifunze kwa walimu wa darasa la awali, la kwanza, la pili na la tatu ili kuwezesha wanafunzi kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.
Joseph ameeleza kuwa mbinu hiyo imesaidia wanafunzi wengi kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa muda mfupi na ametoa wito kwa Manispaa kuendeleza mbinu hiyo.
Aidha, ameeleza kuwa zoezi hilo la ugawaji wa vitu hivyo limeambatana na kauli mbiu isemayo “ulinzi na usalama wa watoto ni jukumu letu sote tupaze sauti kupinga ukatili dhidi ya watoto wetu sote”

Joseph ameendelea kueleza kuwa kwa muda wa Miaka minne mfululizo imekuwa ikishirikiana na manispaa hiyo  kwa kujenga shule za awali katika Shule ya msingi Kibwegere, Malamba Mawili, Goba na Kiluvya kwa gharama za Shilingi milioni 113.3.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kheri James amelipongeza Shirika hilo na kutoa wito kwa wadau wengine kuendelea kuisaidia jamii kama ambavyo wamefanya OCODE.

Kheri ameitaka jamii kutofumbia macho ukatili wa watoto kwani ukatili huo  usipodhibitiwa juu ya watoto wetu wataendelea kunyanyasika. Pamoja na changamoto za maisha zilizopo ni lazima kutenga muda kwa watoto wetu.
“Mapambano dhidi ya ukatili wa watoto ni wajibu wa kila mmoja wetu” Alisema James
Nae Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bi. Leah Linus Sanga ameeleza Shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 2,109  na jumla ya vyumba vya madarasa 11 ya msingi na darasa 1 la awali kutokana na wanafunzi waliopo kuna uhitaji wa vyumba 13 vya madarasa.

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa