• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

MEYA UBUNGO AMSHUKURU RAIS.

Posted on: October 28th, 2021

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo, Mheshimiwa Jaffary Juma Nyaigesha amemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Manispaa hiyo Shilingi bilioni 3.02 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 151 kwa Shule za Sekondari ili kumaliza changamoto ya upungufu wa madarasa katika shule za Manispaa hiyo

Ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa utafanikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2022 kupokelewa na kuendelea na masomo katika mazingira mazuri ya kujifunza na kujifunzia.

Mhe. Jaffary ametoa shukrani hizo leo Oktoba 28, 2021 kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za Maendeleo ngazi ya kata na kuwaeleza wajumbe wa mkutano huo kuwa, ujenzi utafanyika kwa kipindi cha miezi miwili ambapo hadi kufikia 15 Desemba, 2021 madarasa hayo yanapaswa yawe yamekamilika  na tayari kwa matumizi.

"Kutokana na muda wa  utekelezaji  wa ujenzi wa madarasa hayo kuwa mfupi, Mstahiki Meya amewaomba waheshimiwa Madiwani na Watendaji wote kusimamia ipasavyo ujenzi wa vyumba ikiwemo kuzingatia Sheria, kanuni na miongozo katika kutekeleza  miradi hiyo.

"Inatupasa tushirikiane kwa hali na mali ili kusiwe na kikwazo chochote kitakacho kwamisha utekelezaji wa miradi hii ukizingatia muda wa utekelezaji ni mfupi sana"

Mgao wa fedha hizo ni kati ya shilingi trilioni 1.3 za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 uliozinduliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan mwezi Oktoba 10, 2021

Pamoja na kupata fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa 151, pia Halmashauri imepata fedha Shilingi Milioni 420 kwa ajili ya ununuzi wa mashine ya Mionzi ( X-Ray) itakayotumika katika Hospitali ya Wilaya na hivyo kufanya Halmashauri kupata mgao wa Shilingi bilioni 3.44.


Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa