• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

SERIKALI YATATUA MGOGORO SUGU WA ARDHI ENEO LA GOBA KISAUKE

Posted on: July 19th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo  Mheshimiwa Kheri James ametolea maamuzi mgogoro wa  ardhi wa eneo la Goba –Kisauke  katika mtaa wa Tegeta A uliodumu kwa muda wa miaka   mitano na kuelekeza kuwa eneo hilo libaki kuwa  mali ya Mtaa (kijiji).

Akuzungumza na wananchi wa  Mtaa huo  wakati wa mkutano wa hadhara wa kutole maamuzi mgogoro huo  leo julai 19, 2021, alisema maamuzi  hayo yametolewa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi baada ya kufanya uchunguzi wa madai yaliyowasilishwa na familia Tabia Mziwanda na Roman Mosha.

Alisema Tume ya uchunguzi iliyoundwa na serikali kuchunguza mgogoro huo ilibaini kuwa familia ya Tabia  Mziwanda  ambayo ilikuwa ikidai kuwa eneo hilo ni mali yao haikuwa nyaraka zozote zinazo halalisha umiliki wa eneo hilo.

Aliongeza kuwa Tume ilibaini   Bwana Roman Mosha aliuziwa eneo lenye ukubwa ekari nne na  kamati ya kijiji kwa kipindi hicho  kinyume na taratibu za kuuza ardhi ya vijiji inayotaka uuzwaji wa ardhi uridhiwe kwenye Mkutano Mkuu wa Kijiji na si kamati.

‘’Bwana Mosha alileta mkataba wa   mauziano ya ardhi baina yake na kijiji, ambayo inaonesha aliuziwa ekari nne, na katika kamati hiyo mmoja wao ni Mzee mziwanda ambae familia yake inadai kuwa eneo hilo ni mali yao,  serikali imejiridhisha na ushahidi wote uliotolewa na kamati ya uchunguzi kuwa hakuwahi kuwa mmliki wa eneo hilo’’alisema.

Kheri alisema kuwa baada ya Serikali kushirikiki kamilifu katika kuchunguza mgogoro huo na kusikiliza pande zote mbili kihistoria, kimazingira, kinyaraka, viongozi wa Mtaa, na wazee wa Mtaa huo serikali imetoa maamuzi kuwa eneo hilo litabaki kuwa mali ya kijiji (mtaa),na kusimamiwa na Halmashauri ya Manispaa ya ubungo kama sheria ya ardhi inavyoelekeza.

Aliwataka viongozi wa Mitaa kuacha kuuza ardhi kiholela na badala yake  kufuata  taratibu   za kuuza ardhi katika maeneo yao ili kuepusha  migogoro  mbalimbali ya ardhi inayojitiokeza   na kuathiri shughuli mbalimbali za maendeleo.

’’Hakikisheni mnalilinda eneo hili,  mtakapotaka kufanya matumizi mfuate taratibu,  babu zetu walitenga maeneo haya kwaajili ya  kupanua maendeleo  ya mitaa  kama vile kujenga shule, Vituo vya afya, na miradi mingine ya maendeleo hivyo yalindeni  maeneo haya’’  alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Beatrice Dominic ameishuruku Serikali kwa kutoa maamuzi sahihi juu ya mgogoro huo  baada ya kufanya uchunguzi kwa pande zote.

’’Kiukweli sasa nitapumzika naishuruku serikali kutolea maamuzi mgogoro huu ambao ulitusumbua kwa muda mrefu na ulikuwa ukiniathiri mimi pamoja na familia yangu kwa mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa’’ alisema.

Mwenyekiti wa Baraza la Wazee kata ya Goba Yahaya Ndyema ameishukuru Serikali kutoa uamizi wa kurudisha eneo hilo kwa mtaa (kijiji )kwani tangu awali eneo hilo lilikuwa likimilikiwa na  serikali na si watu binafsi wanaoligombania.

“Sisi ndio wazee wa mtaa huu tunajua kuwa eneo hili lilikuwa eneo la kijiji, hawa wote wanaogomabnia wote ni wavamizi tu” alisema mzee Ndyema.

 

 

 

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa