• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

TABOA UBUNGO WAHIMIZWA KUTOKUWA NA OFISI ZA KUKATIA TIKETI NJE YA KITUO.

Posted on: July 6th, 2022

Mapema Leo tarehe 06/07/2022 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg. Beatrice Dominic amekutana na viongozi wa wamiliki wa mabasi (TABOA) wa Kituo cha Mabasi cha Magufuli (Magufuli Bus Terminal) lengo ikiwa ni kuweka mikakati ya pamoja na kudhibiti uwepo wa ofisi za kukatia tiketi nje ya kituo hicho.

Akiongea katika kikao hicho Ndugu Beatrice amewataka TABOA kushirikiana vyema na Manispaa ili kuhakikisha Mabasi yote yanayofanya kazi nje ya Kituo waache kufanya hivyo na badala yake wamiliki wote wa mabasi wanapaswa kuwa na ofisi ndani ya kituo hicho

Beatrice, ameendelea kuelezea kuwa uwepo wa ofisi za kukatisha tiketi nje ya kituo umekuwa ukipelekea Manispaa kupoteza mapato mengi takribani Mil 100 kwa mwezi, lakini pia uhalifu wa kusafirisha madawa ya kulevya umekuwa ukifanyika kwani gari hizo zimekuwa zikifanya safari bila kukaguliwa sababu haziingii ndani ya kituo.

Mbali na hilo Beatrice ameeleza uwepo wa ofisi hizo nje ya kituo cha mabasi umekuwa ukipelekea matatizo mengine mengi ya kihalifu ikiwemo raia kutelekezwa stendi wakiwa na tiketi feki walizopatiwa na ofisi zilizopo nje ya kituo.
 
Aidha, kikao hicho kimeazimia Viongozi wa TABOA wapeleke kwa Meneja wa Kituo hicho orodha ya majina na picha za wafanyakazi wao zikiwemo na  za mawakala wao. Ili Manispaa iwatengenezee vitambulisha maalumu vitakavyo watambulisha ili kusaidia kutatua changamoto zilizopo.
Akiongea Meneja wa Kituo hicho Ndg. Isihaka Waziri amewataka viongozi hao kuacha tabia yakuwapa fedha watu wanawapelekea wateja ambao sio wafanyakazi wao  kitu ambacho kinapelekea kusababisha uingiaji wa watu kiholela ambao wanaweza kuwa wahalifu kituoni humo.

Nae Mwenyekiti wa TABOA Ndg Abdallah Kiongozi ametoa pongezi zake kwa Manispaa na Meneja wa Kituo hicho kwa ushirikiano wanaoupata na kuahidi kuyafanyia kazi yote waliokubaliana kuyatekeleza na wapo tayari kutoa ushirikiano muda wowote pale inapobidi.

#UbungoYetuFahariYetu

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa