• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

VIONGOZI UBUNGO WAJENGEWA UELEWA KUHUSU MFUMOWA ANWANI ZA MAKAZI

Posted on: February 22nd, 2022

 

Viongozi wa Wilaya ya Ubungo wakiwemo Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Madiwani na Wataalam wa Manispaa ya Ubungo wamejengewa uwezo kuhusu mfumo wa anwani za makazi  lengo ikiwa ni kuwa na uelewa wa pamoja katika kulitekeleza zoezi hilo muhimu.

Akiongea wakati wa kufungua mafunzo hayo yaliyotolewa leo Februari 22, 2022 kwa viongozi hao, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mheshimiwa Kheri James ameeleza kuwa mafunzo hayo ni mwendelezo wa utoaji wa elimu kuhusu zoezi hilo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali ambao ndio wasimamizi wakuu wa zoezi.

Tumeitana hapa ikiwa ni utekelezaji wa azima ya Serikali ya kujengeana uwezo kama viongozi tunaowajibika kusimamia zoezi la mfumo wa  anwani za makazi ili kila mtu ajue wajibu wake katika zoezi hili ambalo litatekelezwa kwa muda mfupi yaani kama “operational” tunatamani zoezi hili lifanyike kwa ufanisi na kwa haraka ikiwezekana tuwe wa kwanza kumaliza.

Aidha, Mhe James amewaeleza Madiwani kwa nafasi zao wanawajibu mkubwa sana katika kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo kwa kutoa ushirikiano  wa kutoa taarifa zinazohitajika wakati wa wakusanya taarifa hizo wakifika kwenye nyumba zao kwa ajili ya kuwekwa kwenye mfumo. 

“Tambueni kuwa kufanikisha zoezi hili la mfumo wa anwani ni kufanikisha zoezi la Sensa linalotarajia kufanyika mwaka huu ambapo mazoezi hayo yote yanatekelezwa kwa mujibu wa sheria” alisisitiza Mhe. James”

Akiongea wakati wa kutoa mafunzo hayo, Mratibu wa zoezi hilo JOHN ILOMO alieleza kuwa katika uundaji wa anwani za makazi unahusisha nambari za nyumba, postkodi na  majina ya barabara na kusistiza kuwa utoaji wa majina hayo uzingatie historia ya eneo pamoja na matamshi yanayokubalika na mtaa husika, huku majina yenye itikadi za kidini, kikabila na kisiasa yakikatazwa kabisa kutumika.

Ilomo amesema kuwa utoaji wa  anwani za makazi kwa maeneo yasiyopangika namba zitatolewa bila kufuata mtiririko tofauti na zile zilizopangika ambapo utoaji wa anwani wake utazingatia utaratibu wa namba shufwa kwa upande kulia na namba witiri kwa upande wa kushoto wa barabara.

Pia ameendelea kuwaeleza viongozi hao kuwa maeneo hatarishi au yasiyorasmi kama hifadhi ya barabara, mkondo wa maji au chini ya nguzo ya umeme sheria imekataza kutoa anwani za makazi hivyo taarifa zao hazitaingizwa kwenye mfumo huu.

Kwa upande wao Madiwani wameipongeza serikali kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo yamewapa fursa ya kujua nini cha kuwaeleza wananchi namna ya kushiriki kwenye zoezi hilo muhimu la kitaifa ili likamilke kwa wakati na hatimaye malengo ya serilaki yatimie ikiwemo la kuongeza wigo wa ajira kwa njia ya mtandao, kuwezesha ukusanyaji wa mapato, kusaidia zoezi la sensa kwa wepesi na kupanga vizuri mipango ya maendeleo halisi inayotekelezeka Nchi nzima.

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa