• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Ubungo Municipal Council
Ubungo Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Malengo na dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mipango miji na Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Utumishi na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Maendeleo ya Jamii na Vijana
      • Maji na Usafishaji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
        • Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Masoko
    • Vituo vya Basi
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
      • Ushuru wa Huduma
      • Usajili wa Tax
      • Leseni za Biashara
      • Ushuru wa Hoteli
    • Ujasiliamali
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Ufugaji
      • UJUWA
  • Madiwani
    • Orodha za Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao vya kisheria
    • Ratiba ya Kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi endelevu
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Bronchures
    • Zabuni iliyotangazwa
    • Mpango Mkakati
    • Newsletter
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba

WAFANYABIASHA WAKUBALI KUANZA KULIPA USHURU WA KUSHUSHA NA KUPAKIA

Posted on: August 3rd, 2022

Wafanyabiashara wa kusaga unga Kata ya Manzese Manispaa ya Ubungo kwa hiari wamekubali kuanza kulipa ushuru wa kushusha na kupakia  kulingana na uzito wa gari baada ya kukaa kikao na kukubalina na uongozi wa Manispaa hiyo.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kuwasilisha kwenye kikao hicho mapendekezo ya kuanza kutoza ushuru wa kushusha na kupakia ambapo wafanyabiashara wameishuruku Manispaa kwa kuweka kikao hicho kilichotoa fursa ya kutoa maoni yao kwani wangeweza kutekeleza sheria hiyo bila kutushirikisha.

Akiwasilisha mapendekezo ya ushuru huo, Mweka Hazina wa Manispaa Ndg. George Mzeru amewaeleza wafanayabiashara hao kuwa, Halmashauri imeona vyema kukutana na wafanyabiasha wa mashine za kusaga unga ili kujadili na kukubaliana kwa pamoja viwango rafiki vya kutoza kwenye chanzo hicho ili kila mfanyabiashara alipe badala ya kukwepa.

Baada ya majadiliano ya kikao hicho, wafanyabiashara wamekubali kulipia ushuru huo kwa siku, mwezi na mwaka ambapo kwa siku gari ya tani 2 hadi 3.5 itatozwa shilingi 5000, kwa mwezi 20,000 na kwa mwaka 300,000, kwa gari lenye uzito wa tani Zaidi ya 3.5 mpaka 10 kwa siku 10,000, kwa mwezi 50,000 na kwa mwaka 500,000 huku gari ya Zaidi ya tani 10 itatozwa shilingi 15,000 kwa siku, shilingi 70,000 kwa mwezi na shilingi 700,000 mwaka

“Uhuru wa kushusha na kupakia upo kwa mujibu wa sheriandogo za manispaa, halmashauri ingeweza kutekeleza sheria hiyo bila kuwashirikisha lakini kwa ajili ya kuboresha mahusiano na kujenga ukaribu na wafanyabiashara tumeona tukubaliane viwango rafiki ambavyo kila mfanyabiashara atalipa kwa hiari na bila kumuumiza” alifafanua Mzeru

Kwa upande wake mwenyekiti wa wafanyabiashara wanaosaga na kuuza unga Oscar Munisi ameipongeza halmashauri kwa kuitisha kikao hicho ambacho kimewapa fursa ya kutoa mapendekezo na kukubaliwa na Manispaa “ hii ni heshima kubwa kwetu na tunaahidi kulipa ushuru huu wa kushusha na kupakia  bila kikwazo kwani viwango hivi ni rafiki”

Aidha, Mwenyekiti huyo amesisitiza Manispaa kuendelea kutoa elimu kwa wafanyabaishara juu ya tozo,ada, ushuru na kodi mbalimbali za halmashauri ili kujenga uelewa na utayari wa kulipa kwa hiari kwani mfanyabiashara akielimishwa vizuri hakatai kulipa kodi ya serikali.

Taarifa

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA DEREVA NA KATIBU MAHSUSI July 21, 2022
  • JOINING INSTRUCTIONS KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA UBUNGO MANISPAA 2023. December 28, 2022
  • SELECTION ZA KIDATO CHA KWANZA UBUNGO MANISPAA 2023 December 28, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 02, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAJALIWA AKAGUA MRADI WA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KIBIASHARA MANISPAA YA UBUNGO

    April 20, 2023
  • WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA SHILINGI TRILIONI 9 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    April 14, 2023
  • DC KOMBA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO UBUNGO

    March 31, 2023
  • MADIWANI UBUNGO WAPITISHWA KWENYE MAELEZO YA MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) WA MKOA WA DAR ES SALAAM

    March 28, 2023
  • Tazama zote

Video

BILIONI 1.4 KUJENGA VETA MPYA KIBAMBA | DC KOMBA ATOA SIKU 10 HATI YA ENEO IPATIKANE
More Videos

Viunganishi vya haraka

  • Leseni za biashara
  • Ushuru wa Hoteli
  • Kibali cha ujenzi
  • Sheria ndogondogo
  • Malengo na Dira
  • Muundo wa Uongozi
  • zabuni

Viunganishi linganifu

  • The National Examinations Council of Tanzania
  • TAMISEMI
  • Ministry of Education
  • President office State House
  • National Council for Technical Education
  • Ministry of Finace and Planning

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wanaoingia

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Luguruni Area, Morogoro Road

    Sanduku la Posta: P. 0. BOX 55068 Dar es Salaam

    Telephone: +255 22 2926341

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: md@ubungomc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.Haki zote zimehifadhiwa